Monday, February 22, 2010

ExVIBE organized the first workshop in Songea

Extra Vision 2020 and Beyond (ExVIBE) in collaboration with the Labour Administration and Inspection office of Songea which is an office under the Ministry of Labour, Employment and Youth Development conducted the students workshop on Career Identification and University Course Selection at Songea Club Multimedia Hall on 20th February 2010.
          The Workshop was attended by more than 80 students from different Advanced level Secondary Schools of Songea Municipal. The schools include Songea Boys Secondary School, Songea Girls Secondary School, Ruhuwiko High School, Kigonsera High School and Beroya Secondary School. The workshop was officially opened by acting Regional Administrative Secretary (RAS) of Ruvuma Region. The acting RAS opening speech stressed important issues on employment policy of Tanzania. He said that “65 per cent of the total labour force in Tanzania is youth aged 18-35 thus being among the social group which contributes a lot in the development of this nation.
         Speaking of the workshop itself the organizer and facilitator of that workshop Mr. Frederick Fussi said that “the goal of this workshop is to widen the students understanding on the employment industry nationally and internationally, however the purpose of the workshop is also targeting at improving awareness on Career Identification and University Course Selection”
        The workshop outputs were expected to be Increased information on carrier identification, Increased awareness on the employment industry, Increased awareness on the university course selection, Increased youth empowerment on self employment.
        In order to make this a reality the different renowned and experienced resource persons in Songea presented papers. Eng. Mrs. Mwapongo presented a paper on “self employment and entrepreneurship”. Eng. Kazimoto presented a paper on “Southern Development Opportunities”, Accountant Phinias Opanga presented a paper on “Human Resource Management”, a renowned journalist from TBC Mr.Gerson Msigwa presented a paper on “employment opportunities in Information and Communication Technology”. Other presenters include a labour officer Mr. Oddo Egino Hekela presented a paper on “employment industry” while Frederick Fussi presented papers on “self awareness and university course selection.” The workshop took the duration of one day.

Tuesday, February 16, 2010

UONGOZI NI MAONO

Sifa ya Kiongozi yeyote yule duniani katika nyanja za kila namna ni sharti awe amebeba maono ndani yake ili aweze kuongoza au kuliongoza kundi kwa usahihi mkubwa. Labda tujiulize kwa nini kundi linahitaji kuongozwa?

Hakuna dereva anayeweza kuendesha gari vizuri asipoifahamu barabara aiendeayo au kuufahamu mwisho wa safari yake. Kadhalika kiongozi naye ni lazima afahamu watu anaowaongoza na kutambua kule anakowapeleka. Tunamfananisha kiongozi mzuri na dereva stadi anayelifahamu gari lake kwa ufasaha na kuweza kulichunguza kwa makini na kabla ya hayaanza safari yake hujenga picha akilini mwake juu ya kule anakotakiwa kulifikisha gari lake kwa usalama wa hali ya juu. Dereva huyu lazima kwa namna moja ama nyingine atakuwa amepakia abiria au mizigo ndani ya gari lake. Uwezo wa dereva kupiga picha ya safari nzima tungu mwanzo wa safari hadi mwisho wake humfanya dereva kuwa na sifa ya maono. Hatumtegemei dereva huyo kufanya tofauti na maono yake. Maono yake ni kuliendesha gari lake kupitia barabara fulani kwa mwendo fulani na kufika sehemu husika ndani ya muda uliopigiwa mahesabu. Kuzifahamu changamoto zitakazomkabili njiani wakati wa safari nayo pia ni sifa ya dereva huyu mzuri mwenye maono.

Kadhalika kwake kiongozi mwenye maono huwafahamu watu wake vizuri, huzijua changamoto za watu wake na yeye hufahamu namna bora ya kuzikabili hizo changamoto ili aweze kulipigisha hatua kundi lake. Kiongozi bora ni mwenye maono mithili ya mchungaji wa kondoo. Mchungaji wa kondoo huwatoa zizini asubuhi hali akifahamu aina ya malisho sahihi kwa ajili ya afya ya kondoo wake. Hufamu vyema mto ule wenye maji safi na salama ambayo kondoo wake watayanywa wakiwa malishoni. Wanyang’anyi wajaposogelea kundi la kondoo wake yeye husimama kidete kuwatetea kwa kuwa ana maono ya kuwarudisha salama katika zizi lile lile alilowatoa asubuhi.

Uongozi ni maono, pasipo maono uongozi huwa mgumu na mafanikio habakia kuwa ndoto miongoni mwa kundi ama watu wanaoongozwa. Kiongozi hubeba maono ambayo hushikwa na wale anaowaongoza. Uwezo wa kundi kuyashika maono ya kiongozi wao ndio uwezo wa kundi kufanikiwa na kuwa salama nyakati zote. Wapo watu ambao sio viongozi lakini wanaongoza. Watu wa namna hii hutawaliwa na nyakati zisizokuwa na mafanikio yaliyo dhahiri. Viongozi hawa huwa na sifa ya kukosa maono na uzoefu anonesha kuwa viongozi hawa huliyumbisha kundi wanaloliongoza. Uongozi ni maono, maono hayo hubaki kuwa msaada mkubwa kwa kuwa watu au kundi linaloongozwa na kiongozi mwenye maono hufanikiwa kwa kasi ya ajabu kwa sababu imo siri kubwa ndani ya kiongozi aliyebeba maono sahihi na maono hayo yakashikwa na kundi lake.

Friday, January 1, 2010

TAIFA LENYE MAONO NA WATU WENYE MAONO


Ukuaji wa Taifa lolote lile duniani unategemea na aina ya maono ya watu au wananchi wanaoishi ndani ya hilo Taifa. Maono ni uwezo wa mtu kuona mambo yajayo kabla ya wengine, kuyaona sana kuliko wengine na kuona mbali zaidi ya wengine.


Ili Taifa likue linahitaji kuwa Taifa lenye maono ya hali ya juu. Na ili maono yawepo panahitajika wawepo watu wachache na sio wote wanaoweza au wenye uwezo wa hali ya juu wa kuona na kubeba maono ya Taifa hilo. Kwa mfano kabla Tanganyika haijapata uhuru palikuwepo na watu wachache wenye uwezo mkubwa wa kuona mbali na kuweza kubeba maono ya Taifa. Watu hawa ndio waliokuwa viongozi na vinara wa kuung’oa utawala Kiingereza katika ardhi ya Watanganyika na kuamua kuunda upya Taifa lao.
 Kimsingi zipo awamu nne tangu Taifa letu lipate uhuru. Katika awamu hizi nne kumekuwepo na matarajio ya kuwa tungekuwa na watu wachache wenye maono ya kulijenga Taifa letu kama ilivyokuwa kwa kipindi cha Mwl. J.K. Nyerere. Mfano mzuri Mwl. Nyerere alikuwa mtu mwenye maono. Mwalimu aliamini katiaka maono yake kwa Taifa na kuwa mstari wa mbele kuongoza Watanzania wenzake. Si kweli kwamba Mwl. Nyerere aliweza kuyafanya mambo yote peke yake la hasha alikuwa na wasidizi wake wa Karibu ambao nao pia waliamini ndani ya maono ya Mwalimu na kuyashika hayo maono. Kwa mantiki hii sasa tunagundua kuwa Mwalimu alikuwa na maono na wasaidizi wake walijifunza ama kuyashika au kuyakataa. Enzi hizo ili Taifa likue ilitegemea ni namna gani wasaidizi wa Mwalimu walikubali kuyashika maono na kuyatendea kazi. Katika kipindi hicho wapo wale walioyashika maono na kuyatendea kazi na wapo baadhi ambao hawakuona umuhimu wa kuyashika maono.

Uwezo wa Taifa kukua unategemea ni namna gani watu wa Taifa hilo wanayashika maono ya kiongozi wao na kuyatendea kazi. Ili Taifa likue linahitaji maono sahihi ya kiongozi wa Taifa. Si kila mtu tunayemwita kiongozi anaweza kubeba maono ndani yake. Na si kila mtu anaweza kubeba maono. Ili kuweka uwiano katikati ya Taifa lazima awepo mtu mmoja ambaye ndani yake anakuwa amebeba “maono ya Taifa lake”. Maono ya Taifa huanza ndani ya mtu mmoja na watu wa Taifa lake huwa watu wenye maono kwa sababu tu wameyashika maono ya mtu mmoja miongoni mwao. Kukikosekana mtu mmoja mwenye maono Taifa hupitia katika vipindi vigumu tofauti na aina ya ugumu unaojitokeza endapo Taifa lina mtu aliyebeba maono na wengine kuyashika. Taifa letu Tanzania linahitaji “maono sahihi” kutoka kwa “mtu sahihi” na Watanzania wote wanahitaji kuyashika maono hayo ili Taifa lao lipige hatua.

Taifa letu Tanzania bado linatembea ndani ya maono ya mtu mmoja ambaye bahati nzuri alishamaliza kazi yake na hivyo maono hayo kufikia ukomo kiuhai. Kuna “maono hai” (active vision) na “maono yaliyokufa” (dormant vision). Tanzania kwa sasa haina “maono hai”. Ni vigumu mtu kuamini kama Tanzana ya sasa haina “maono hai” Lakini ukweli unabakia kuwa Taifa letu kwa sasa halina maono hai. Huhitaji kuwa na elimu kubwa kutambua kuwa Taifa linatembea ndani ya “dormant vision”. Chunguza kasi ya ukuaji wa kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na wa Taifa na kasi ndogo Maendeleo ya jamii utagundua kuwa hatua tulipo sasa ilibidi tuipige zaidi ya miaka 30 iliyopita.Tunaweza kujivunia hatua ile tuliyoipiga sasa, vyema, lakini hatustahili kujivunia kwa sababu Tanzania ni zaidi ya mafanikio yote tuliyonayo sasa. Tanzania haistahili kuwa ilipo sasa. Ipo njia sahihi ya kuifikisha Tanzania inapotakiwa kuwapo. Upo umuhimu wa kila Mtanzania kugundua kuwa hatustahili kuwa hapa tulipo. Tunayo stahili yetu. Na ili kuifikia stahili yetu sharti tukubali kulipia gharama za kuwa na maono hai(active vision). Na huu ndio mwanzo mpya wa maono hai (the new beginning of an active vision).